![]() |
Benki kuu ya Tanzania |
Miongoni mwa majukumu ya Benki Kuu ya
Tanzania (BOT) ni kusimamia kikamilifu masuala mbalimbali ya kibenki na
kifedha ikiwemo masoko ya fedha za kigeni, mifumo ya malipo yote ni
kuhakikisha uchumi nchi unakuwa na kuwa na manufaa kwa kila mtanzania.
Kwa
mujibu kutoka benki hiyo inaeleza kuwa Juni 14 mwaka huu BOT
inasherekea miaka 50 tangu kuanzishwa kwake kama Benki Kuu ya Taifa.
Benki
kuu ilianzishwa kwa sheria ya mwaka 1965 (The Bank of Tanzania Act 1965)
na ilianza kufanya kazi rasimi14 Juni mwaka 1966.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo majukumu na shughuli za Benki Kuu na muundo wake
umekuwa ukibadilika kulingana na mabadiliko ya sera za kijamii na
kiuchumi nchini pamoja na maendeleo ya kiuchumi na mfumo wa fedha kikanda
na kimataifa.
Katika kipindi cha kuanzia mwaka 1967 hadi 1991, BOT
ilijikita zaidi kufanikisha juhudi za Serikali katika kutimiza malengo ya
kukuza uchumi katika mlengo wa ujamaa na kujitegemea.
Kwa wakati huo sera ya fedha ilitegemea maelekezo kutoka
Serikali Kuu ambapo Sera ya fedha ilikuwa ikitekelezwa kwa kutumia miongozo ya
fedha na mikopo na ile ya fedha za kigeni sambamba na udhibiti katika
riba na upatikanaji wa mikopo na fedha za kigeni.
Hata hivyo hali hiyo, ilipelekea kudhoofu kwa mihimili
mikuu ya uchumi sambamba na ongezeko kubwa la ujazi wa fedha, mfumuko wa
bei, kuporomoka kwa thamani ya Shilingi na kudhoofu kwa kasi ya ukuaji wa
uchumi.
Aidha
taarifa hiyo inaeleza kwamba kutokana na udhaifu huo uliojitokeza, Serikali
ilichukua hatua za makusudi kuunusuru uchumi mwishoni mwa miaka ya 1980,
kwani mwaka 1986 juhudi mbalimbali zilifanyika katika kuendeleza shughuli
za kufufua uchumi.
Mwaka
1988 moja ya hatua serikali ilizochukua ilikuwa ni kuunda Tume ya Uchunguzi
chini ya Gavana Charles Nyirabu ili kushughulikia matatizo katika sekta ya
fedha.
Kwa
kuzingatia mapendekezo ya tume hiyo, iliundwa Sheria ya benki na Taasisi za
fedha ya mwaka 1991 (Banking and Financial Institutions Act) kufungua njia kwa
sekta binafsi kushiriki katika kuendeleza sekta ya fedha.
Sanjari
na hayo sheria ya Benki Kuu ya mwaka 1995 (Bank of Tanzania Act) ilitungwa na
kuiwezesha BOT kuondokana na majukumu mengi na kujikita katika jukumu moja kuu
la usimamizi wa utulivu wa bei.
Mabadiliko
haya ambayo yalikuwa na malengo mazuri ya kukuza uchumi na kuwa na faida katika
nyanja mbalimbali za kimaendeleo na kulisaidia taifa la tanzania kusonga mbele
katika uchumi.
Baada ya mabadiliko mafanikio katika
utekelezaji wa sera mbalimbali,
hususan, sera ya fedha kama
inavyojionyesha katika kushuka kwa kasi
ya mfumuko wa bei na ukuaji wa
uchumi.
Kwa
mujibu wa taarifa kutoka benki kuu mfumuko wa bei ulipungua
kutoka
wastani wa asilimia 30 katika miaka ya 1980 hadi chini ya asi
limia 10 kwa miaka ya hivi karibuni
ambapo, ukuaji halisi wa uchumi
umekuwa ukiongezeka kwa wastani wa
asilimia 7 katika kipindi cha m
uongo mmoja na nusu uliopita,
sambamba na ongezeko la mikopo kwa
sekta binafsi.
Aidha
upatikanaji wa huduma za kifedha umeongezeka na kufikia
asilimia 79 ya
idadi ya watu wazima hapa nchini wanapata huduma
rasmi za
kifedha katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Ikumbukwe
kuwa kabla ya kuanzishwa kwa Benki Kuu ya Tanzania, kazi kuu ya benki nchini
Tanzania (wakati huo Tanganyika) ilifanywa na mashirika mbalimbali.
Mathalani
kampuni ya Kijerumani ya Afrika Mashariki (Germany East African Company) ambayo
ilikuwa inasimamia koloni la Kijerumani la Afrika Mashariki ndiyo iliyokuwa na
wajibu wa kudhibiti ujazi wa fedha mpaka mwaka 1903.
Wakati
huo, Benki itwayo Deutsch-Ostafrikanische Gesellschaft ilipewa jukumu la
kuchapisha sarafu zilizoanza kutumika Tanganyika mwaka 1905.
Jukumu
hilo baadaye lilichukuliwa na Serikali ya Ujerumani mpaka mwaka 1918 na sarafu
iliyokuwa inatumika wakati huo ilikuwa inaitwa Rupia
.
Taarifa
kutoka BOT inaeleza kuwa kwa upande wa Zanzibar, jukumu la fedha lilikuwa chini
ya Utawala wa Uingereza,ambapo jukumu la kusimamia ujazi wa fedha lilisimamiwa
na serikali ya Uingereza.
Hivyo
kipindi cha pili ni baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia (1914-18), ambapo
Uingereza ilitawala Tanganyika na Zanzibar, mfumo wa malipo uliokuwa unatumika
wa fedha taslimu na hundi zilizotolewa na mfumo wa benki za kikoloni ambao
ulishamiri hasa kwenye miji mikubwa.
Mwaka
1919 sarafu ya Afrika Mashariki ilianzishwa kwa ajili kudhibiti ujazi wa
fedha katika makoloni ya Uingereza ya Afrika Mashariki na nchi jirani.
Mwaka
1921 sarafu ya Rupia iliondolewa na kuanzishwa mfumo wa Poundi pamoja na
Shilingi.
Taarifa
hiyo ya benki inaeleza kuwa historia ya Sera ya Fedha Tanzania ilianza
mwaka 1919 wakati Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilipoanzishwa kwa lengo la
kusimamia ujazi wa fedha katika nchi za Kenya, Uganda na Tanganyika.
Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki ilikuwa mtazamaji wa
fedha na hasara yake ilikuwa kutokuwa na uwezo wa kusimamia sera ya
fedha.
Tangu
kuanzishwa kwa BOT, sera ya fedha nchini imekuwa ikibadilika mara kwa mara kwani
katika kipindi cha mwaka 1960 hadi 1970, sera ya fedha ya Benki Kuu ilitegemea
maelekezo kutoka serikali Kuu kupitia miongozo ya fedha na mikopo na ile ya
fedha za kigeni iliyoanzishwa mwaka wa 1971/72.
Mipango
ya matumizi ya fedha za kigeni iliandaliwa kulingana na vipaumbele vya taifa.
Sera ya fedha ya BOT ilitegemea zaidi maelekezo kutoka serikalini. Katika
kipindi hicho hakukuwa na soko la mitaji wala la fedha.
Aidha
zana ya fedha pekee iliyokuwepo ni dhamana za Serikali ambazo zilitolewa kwa kampuni
ya Bima ya Taifa, mifuko ya hifadhi ya Jamii na Benki ya Posta. Benki
zilizokuwa zinamilikiwa na Serikali ndizo zilitawala mfumo wa kibenki na riba
ilikuwa inapangwa na utawala.
Udhibiti
huo wa moja kwa moja ulionekana kuwa ni chanzo kimojawapo cha matatizo ya
uchumi yaliyotokea mwanzoni mwa miaka ya 1980 kutokana na kuwa na thamani kubwa
kuliko uhalisia wake.
No comments:
Post a Comment