Wananchi washirikishwe utoaji vibali kwa wawekezaji: Simbachawene - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, June 14, 2016

Wananchi washirikishwe utoaji vibali kwa wawekezaji: Simbachawene



 
Waziri wa nchi Ofisi ya rais Twala za Mikoa na Serikali za mitaa George Boniface Simbachawene, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Dar es Salaam jana, wakati wa mdahalo ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi wa Institute juu ya maswala ya Uwekezaji na Vibali vya wananchi uwekezaji
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais ,Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa ,George  Simbachawene amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa Sheria, na Mikataba ya uwekezaji baina ya Serikali na Wawekezaji ni lazima wananchi nao  washirikishwe kikamilifu katika utoaji wa kibali hicho cha uwekezaji ili nao waweze kunufaika.
Akizungumza Dar es Salaam jana,wakati wa Mdahalo unaohusu masuala ya uwekezaji baina ya serikali,wawekezaji na wananchi ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi,Simbachawene alisema licha ya kuwepo kwa mikataba baina ya wawekezaji na Serikali pia Wananchi wanapaswa kushirikishwa,ikiwa ni sehemu moja wapo ya wao kupata maendeleo.
Alisema wananchi wanaozungukwa na rasilimari mbalimbali wanapaswa kuwa  sehemu ya maendeleo kutokana na uwekezaji katika eneo husika na kuona faida kwa uwazi tangu siku ya kwanza muwekezaji anapoanza kuwekeza.

 “Hapa kuna wadau mbalimbali wamekutana katika mdahalo wa kujadili mambo mbalimbali ya maendeleo yanayohusu nchi za Afrika katika shughuli  zake ikiwemo katika masuala ya uchimbaji wa madini na mafuta na kuona ni namna gani jamii inavyofaidika na kunufaika na wawekezaji wanaowekeza katika maeneo yao,”alisema

Simbachawene alisema wananchi  wanahaki ya kutoa kibali kwa wawekezaji,na kuwakubalia kufanya shughuli zao katika maeneo yao au la.
  
Alisema Tanzania ina nguvu ya kiuchumi kutokana na uwepo wa rasilimali zake ambapo  takwimu za mwaka 2015  zinaonyesha hadi sasa ni asilimia 10 tu za madini nchini zimechimbwa huku asilimia 90 zikiwa bado hazijachimbwa katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Aidha alisema endapo watanzania watakuwa makini katika kutunza rasiliamari zake itasaidia kuimarisha uchumi imara katika nchi.

“Serikali na wananchi tushirikiane kwani fursa tulizonazo ni nyingi mpaka sasa hakuna kilichoharibiwa inatupasa tutumia elimu ili  kurekebisha makosa tuliyokuwa nayo katika mikataba ya uwekezaji,
 Alisema zipo sheria mbalimbali zinazosimamia uchimbaji na uvunaji wa rasilimali ya madini na Mafuta,ambapo mara nyingi rasiliamri hizi zinapopatikana kuna tokea na fujo nyingi kutokana na wananchi kutoshirikishwa juu ya uwekezaji unaofanyika katika maeneo yao.

Aidha alisema rasilimari zinapovunwa na wawekezaji wananchi wanakuwa wanaachiwa madhara makubwa hivyo elimu inapaswa kutolewa kwa wananchi pindi mwekezaji anapokuja kuwekeza ili pawepo na uwazi zaidi.
“Wataalama duniani wamekaa na kuendelea kufikilia zaidi ya sheria zaidi si kwamba mtu anaweza kuendesha uvunaji wa rasirimali ya mafuta na Madini kwa kutumia sheria,ni lazma kuwepo kwa kipengele cha wananchi kuwa na kibali cha makubaliano kati ya wananchi na muwekezaji,”alisema

Alisema uwekezaji unaofanywa na wawekezaji wengi unasababisha kuwepo kwa migogoro mingi ambayo inatokana na kutoingia mikataba rafiki na wananchi wa eneo husika.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot