Moto kuwawakia waficha Sukari - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, June 14, 2016

Moto kuwawakia waficha Sukari


Serikali imewatangazia kimbunga cha moto mawakala wa sukari na wafanyabiashara wa rejareja mkoani Arusha wale wote watakaoficha bidhaa hiyo baada ya kiwanda cha TPC kuanza uzalishaji wake
Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Said Mecky Sadiki, alisema sukari hiyo itakapoingia sokoni, wasambazaji na wafanyabiashara wa rejareja yeyote atakayeuza tofauti na bei elekezi ya serikali atafikishwa kwenye vyombo vya sheria.

 

Sadiki alisema kwa mfanyabiashara yeyote atakayekuwa na sukari kutoka nje kwenye duka au ghala lake mara baada ya sukari ya TPC kuingia sokoni, atalazimika kuuza bei elekezi ya serikali bila kujali bidhaa hiyo imetoka wapi.

“Kiwanda cha TPC kitaanza uzalishaji wa sukari kesho, na watahadharisha mawakala na wafanyabiashara wa rejareja, kutojiingiza kwenye mchezo mchafu wa kuhodhi bidhaa hiyo. Hatutaki kusikia kisingizio kuwa sukari inayouzwa bei ya juu inatoka nje,…tunachotaka sukari iuzwe bei elekezi ya serikali ya shilingi 1800 ,” alisema Sadiki.

Sadiki alisema bei ambayo kiwanda cha TPC itawauzia mawakala inajulikana na serikali, hivyo kinachotakiwa kwa mawakala hao ni kuongeza asilimia 3.25, pamoja gharama nyingine kama usafiri na sio vinginevyo, ili wananchi waweze kuipata kwa bei elekezi ya serikali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot