![]() |
| Wavulana wanne wakiwa wamevaa sketi kama unifom za shule huko nchini uingereza |
Na Mwandishi Wetu
Wavulana wanne katika shule moja nchini Uingereza wameeenda shuleni wakiwa wamevaa sketi kulalamikia hatua ya mwalimu kuwaadhibu kwa kuvalia kaptura siku yenye joto kali zaidi nchini humo.
Wanafunzi hao wa darasa la mwaka wa tisa katika shule yaLonghill eneo la Rottingdean, Sussex Mashariki, walikuwa miongoni mwa wanafunzi 20 wavulana waliovalia kaptura za kuvaliwa wakati wa mazoezi badala ya suruali ndefu.
Baadhi walifukuzwa shuleni Jumanne na wengine kutengwa hadi siku iliyofuata. Waliokubali kuvua kaptura hizo na kuvalia suruali ndefu hawakuadhibiwa.
Lakini badala ya kuvalia sare kamili ya wakati wa masomo, kama walivyokuwa wameagizwa, wanafunzi wanne walirejea shuleni Alhamisi wakiwa wamevalia sketi.
![]() |
| Michael Parker, mmoja wa wanafunzi, akiwa na kaptura na akiwa na sketi |
Mwalimu mkuu Kate Williams aliwaambia wanaweza kuvalia mavazi yoyote, mradi yawe ni sehemu ya sare iliyokubalika shuleni.
Wanafunzi hao walivaa sketi kwa siku mbili mfululizo ikiwa ni kujirisha kwa kile walichokiona kuwa ni sahihi.




No comments:
Post a Comment