Ujumbe wa Zitto Kabwe kwa Rais Magufuli baada ya kuwa Mwenyekiti wa CCM - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Sunday, July 24, 2016

Ujumbe wa Zitto Kabwe kwa Rais Magufuli baada ya kuwa Mwenyekiti wa CCM

 
Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe
Na Mwandishi wetu.
 
Baada ya Rais Magufuli kutangazwa kuwa ameshinda na kuwa ndiye Mwenyekiti wa tano wa CCM Taifa akichukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Rais wa awamu ya nne, Dkt Jakaya Kikwete, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi Mkuu wa ACT- Wazalendo ameandika haya kwenye ukurasa wake wa Facebook;-
 
“Napenda kumpongeza Rais John Magufuli kwa kuchaguliwa kwake kuwa Kiongozi wa Chama chake cha CCM akiwa Mwenyekiti wa Tano chama hicho. CCM imeendelea kudumisha utamaduni wa kukabidhiana Uongozi kila baada ya muda.
 
Jambo ambalo ni la kujifunza hasa kwa vyama vya Siasa nchini na barani Afrika. Nataraji kwamba Rais na Mwenyekiti mpya wa CCM ataona umuhimu wa Vyama vya Siasa kuendelea kufanya Siasa bila vikwazo na kwa mujibu wa Sheria za Nchi yetu.
 
 Demokrasia inaimarisha Amani kwa kupaza sauti za HAKI. Karibu kwenye changamoto za kuongoza Vyama vya Siasa ndugu Rais.” 

Pia alisema hivi
"Zanzibar sasa iwe ajenda ya kudumu kwa Vyama vyote vya Siasa vinavyosimamia HAKI. Rais Magufuli hawezi kukwepa tena suala la Zanzibar kwani sasa ni Mwenyekiti wa Chama chake. Hana excuse tena. Suala la Zanzibar sio la CUF peke yao, ni suala letu sote. Shime wana demokrasia"



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot