Zaidi ya watu 50 wauawa na kimbunga China - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, June 23, 2016

Zaidi ya watu 50 wauawa na kimbunga China


Ni moja kati ya maeneo yaliyoathirika kutokana na mvua pamoja na kimbunga huko nchini China.
Na Carlos Nichombe

Vyombo vya habari nchini China vinasema kuwa zaidi ya watu 50 wameauwa kufuatia kutokea kimbunga na mvua kubwa katika mkoa ulio mashariki mwa nchi wa Jiangsu.

Katika maeneo ya mji wa Yanchen kimbunga hicho kilisababisha nyumba kuporomoka na kung'oa laini za umeme.

Sehemu nyingi za nchi zimekumbwa na mvua kubwa wiki hii. Mafuriko kati kati mwa China yamesababisha karibu watu 200,000 kuhama makwao.

Mamlaka ya Hali ya hewa ya nchi hiyo imetahadharisha wananchi kuwa makini kwa sasa kutokana na hali ya hewa kutokuwa nzuri.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot