TBS yateketeza mchele Dar - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, June 27, 2016

TBS yateketeza mchele Dar

mchele

Na Mwandishi Wetu

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS)limeteketeza  tani mbili za mchele  wa Pakistani zilizokamatwa katika bandari ya Dar es Salaam  ukiwa unatokeo Zanzibar.

Akizungumza wakati wa uteketezaji wa bidhaa hizo jijini Dar es salaam jana, Ofisa udhibiti ubora wa TBS, Grangay Masala alisema  mchele huo  ulikamatwa  May 12 mwaka huu bandari ya Dar es Salaam  ukitokea  Zanzibar.

Alisema  baada  ya kukamata Mchele huo  ambao ulikuwa tani 6  wenye  thamani  ya sh. milioni 10 walienda kupima katika maabara ya TBS na  kugundua kuwa tani mbili zimeshaisha muda wake wa matumizi.

Alisema mchele huo  umetokea  Pakistani kupitia bandari ya Zanzibar hivyo  kutokana na muda wake wa matumizi kwisha  unaweza kuleta madhara  kwa watumiaji.

"TBS imepima mchele huo katika maabara zake na kujiridhisha kuwa mchele huo haufai kwa matumizi ya binadamu hivyo  tunateketeza kuepusha madhara kwa wananchi,"alisema Masala.

Alisema  mchele huo endapo ungetumika  unaweza kusababisha madhara ya kiafya  kwa binadamu kama  kupata  fangasi wanaotengeneza sumu  mwilini, kansa ya ini na  kudumaa kwa watoto.

Kwa upande wake Ofisa husiano wa (TBS)Neema Mtevu, amewataka wafanyabiashara kuhakikisha wanaingiza bidhaa zenye ubora na wawe walinzi tosha wa kuhakikisha bidhaa hafifu haziingizwi nchini.

Pia alisema  kuwa wafanyabiashara  wanatakiwa kufuata taratibu  za nchi  katika  uingizaji  wa bidhaa na kuepuka kuingiza bidhaa zilizo chini ya kiwango.

Alisema TBS  wapo  kila eneo kuhakikisha wanadhibiti  bidhaa  zilizo chini ya kiwango kuhakikisha  haziingii nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot