Halmashauri zahimizwa kutenga asilimia 10 - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, June 16, 2016

Halmashauri zahimizwa kutenga asilimia 10

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene (katikati) akikata utepe ikiwa ni ishara ya ufunguzi wa Tawi jipya la Benki ya DCB Plc Benjamin Mkapa City, Dar es Salaam juzi. Wengine ni baadhi ya viongozi wa benki hiyo na Jiji. Wa pili (kulia) ni Mkurugenzi wa benki hiyo, Edmund Mkwawa. Nyuma ya Waziri ni Mwenyekiti wa Bodi ya wakugenzi, Balozi Paul Rupia, Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Profesa Lucian Msambichaka, Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando. Kulia ni Meya wa Jiji, Isaya Mwita. Picha na Charles Lucas

Na Grace Ndossa

HALMASHAURI zote nchini zimetakiwa kuhakikisha zinatenga fedha asilimia 10 za vijana na wanawake kutoka kwenye mapato ya ndani kama walivyoagizwa.

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam jana na  Waziri  wa nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene alipokuwa akizindua Tawi jipya la Benjamin Mkapa city la Benki ya Biashara ya (DCB).

Alisema kuwa Halmashauri  pamoja na kutenga fedha hizo bado ni ndogo kwani  asilimia  10 haijafika  hivyo lazima wafanye hivyo kama walivyoagizwa.

"Fedha zilizotolewa na Ilala  milioni 700 kwa ajili ya vijana na  wanawake na  fedha zilizotolewa na  Wilaya ya Kinondoni  milioni 997 siamini kama ndo asilimia kumi ya mapato ya  ndani hivyo  bado wanatakiwa kutekeleza agizo hilo,"alisema Simbachawene.

Hata hivyo aliipongeza benki ya DCB kwa kujitahidi kupiga hatua  na  kutoa gawio kwa wanahisa  pamoja na mtaji wao kuongezeka kutoka  bilioni  1.1  tangu mwaka 2002 hadi kufikia  bilioni 32.

Alisema  halmashauri zote zinatakiwa kukaa na kukubalina waweze kuweka fedha zao huko kama walivyokubaliana awali kuanzishwa kwa benki hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Edimund  Mkwawa alisema Benki  imeweza kupata  faida na kutoa gawio kwa wanahisa  kwa kipindi cha miaka kumi mfululizo ambapo kwa mwaka 2015  bilioni 11.73 zimetolewa kama gawio ikilinganishwa na  sh milioni 215.4 zilizotolewa mwaka  2006

Alisema benki hiyo inatoa bilioni 1.55kama  gawio kwa wanahisa wake kwa faida ya mwaka 2015 ambapo  ametoa hundi kwa baadhi ya  wanahisa.

"Mtaji wa benki umeongezeka kupitia uuzaji  hisa za haki  na  hisa  za awali kupitia soko la hisa la Dar es salaam ambapo DCB imekuwa  benki ya kwanza nchini kujiunga na soko hilo Novemba  2008,"alisema Mkwawa.

Hata hivyo alisema kuwa  DCB imekuwa ikipata  faida tangu mwaka 2004 ambapo faida ilikuwa milioni 447.6 na kwa mwaka 2015 faida baada ya kodi imefikia  bilioni 3.1

Alisema kuwa tawi  walilozindua  ni la tisa kwa  hapa Dar es Salaam na wanaendelea  kuboresha na kusogeza huduma  za kibenki karibu na wananchi  .

Pia DCB inatoa  sehemu ya faida  inayopatikana kusaidia jamii inayoizunguka na  kwa mwaka huu tunatoa madawati 300 yenye thamani ya  sh milioni 39 kwa shule za msingi Mkoa wa Dar es Salaam ili kukabiliana na uhaba wa madawati.

Mwisho

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot