![]() |
Msahambuliaji wa zamani wa Misri, Mohamed Aboutrika |
Aboutrika anashutumiwa kuwasaidia kifedha kikundi cha Brotherhood, ambacho mamlaka za Misri kimewaweka kwenye kundi la magaidi kutokana na matukio mbalimbali wanayoyafanya.
Mnamo mwaka 2012, Aboutrika alimpigia kampeni ya urais, Rais wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Morsi, ambaye ni mwanachama wa Brotherhood.
Kwa mujibu wa sheria mbalimbali za Misri, mtu yoyote anayewekwa kwenye listi ya ugaidi, hufungiwa kusafiri na passport yake pamoja na mali zake hushikiliwa.
Kwa upande wake Mwanasheria wa Aboutrika, Mohamed Osman, alisema mteja wake hajatiwa hatiani wala hajapewa taarifa rasmi juu ya mashtaka wanayomtuhumu juu yake.
No comments:
Post a Comment