AMANA bank wazindua kituo cha mawasiliano - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, July 21, 2016

AMANA bank wazindua kituo cha mawasiliano


Meneja wa Kituo cha Huduma kwa Wateja Bw. Juma Msabaha akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uzinduzi wa kituo cha huduma kwa wateja kilichozinduliwa hii leo Makao Makuu ya Benki hiyo, Golden Jubilee towers Dar es Salaam.
Na Sekela Mwambene.

KATIKA kusogeza huduma zake karibu,Benki ya Amana imezindua Kitengo cha huduma kwa wateja kitakacho mwezesha mteja kupata huduma na taarifa zinazo husiana na benki hiyo.

Akizungumza Dar es Salaam jana,Meneja Mfawidhi huduma kwa wateja katika  Benki hiyo  Juma Msabaha alisema kuwa  lengo ni kusogeza huduma kwa wateja,kupokea maoni mbalimbali kuhusiana na huduma pamoja na maboresho zaidi.

Alisema kituo hicho kitasaidia kuboresha  taarifa  za  huduma za moja kwa moja ikiwemo  ATM,huduma za kibenki kwa njia ya Simu,pamoja na miamala ya kifedha ambazo zinatumiwa na wateja.

"Lengo la huduma hii itaongeza mahusuasiano mazuri baina ya mteja na benki ,hivyo wateja watumie kituo hicho kama njia sahihi ya kufikisha malalamiko,maoni na maboresho kwa benki yetu"alisema Msabaha.

Kwa Upande  Mkurugenzi wa Biashara wa benki hiyo Munir Rajab alisema kwa sasa wanampango wa  kuongeza matawi  katika maeneo mbalimbali ya nchi ili kuongeza wigo mpana wa kuwahudumia wateja.

Alisema wanampango wa kufungua matawi mawili ikiwemo Zanzibar ambapo benki hiyo haikuwepo kwa upande wa visiwani na bara itafunguliwa moja katika mkoa wa Tanga.

"Kwa sasa  benki yetu inamatawi saba ambapo matano yapo katika mkoa wa Dar es Salaam ,Mwanza moja na Arusha  hivyo wateja wetu waendelee kutumia huduma zetu kwani tunatoa huduma zenye ubora tofauti na benki nyingine"alisema Rajab

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot