Khadija Kopa awachana wasambinungwa - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, June 28, 2016

Khadija Kopa awachana wasambinungwa

Malkia wa Mipasho nchini, Khadija Kopa

MALKIA wa mipasho nchini, Khadija Kopa amefunguka na kusema kuna ubaya pale  mwanamke mwenye umri mkubwa kutoka kimapenzi na mtoto chini ya miaka 18, ila kijana akishavuka umri huo hakuna cha kushangaza.

Kopa alifunguka kuwa  haoni ajabu wanawake wenye umri mkubwa kutoka kimapenzi na vijana wadogo, ilimradi kuna mapenzi ya dhati kati yao.

Malkia huyo alisema  kuwa  mapenzi ni maridhiano, hayachagui umri na hufanana mno na majani yanayoweza kuota mahali popote.

“Huwa nawashangaa watu wanaosema mapenzi ya namna hiyo ni ajabu, kama kuna maridhiano baina yao uajabu wao unatoka wapi? Waache kufuatilia yasiyowahusu kama wenyewe wanapendana iweje wewe utie maneno,” alipasha  Kopa.

2 comments:

  1. Hapo umenena mamaaaaaaaaaaaaaaa

    ReplyDelete
  2. Xema malkia wa Mipasho jaribu basi hata kuchagua watuwa rika lako kidogo usichukue watoto wadogo tu

    ReplyDelete

Post Top Ad

Your Ad Spot