Chris Brown apelekwa mahakamani - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, June 30, 2016

Chris Brown apelekwa mahakamani

Mwnamuziki wa Zamani Suge Knight
Na Mwandishi Wetu
 Suge Knight amemshtaki mwanamuzki mwenzake wa R& B Chris Brown mahakamani pamoja na mmiliki wa klabu moja ya usiku nchini Marekani kufuatia ufyatulianaji wa risasi uliotokea katika klabu hiyo mwaka 2014.

Mwanamuziki huyo wa zamani alipigwa risasi mara saba katika hafla ya mwanamuziki Chris Brown.

Kesi hiyo iliyowasilishwa katika mahakama ya Los Angeles inamshtaki Chris Brown na klabu ya West Hollywood Ckub 1 Oak kwa kushindwa kuweka usalama wa kutosha na kumruhusu mtu mmoja aliyejihami kuingia katika kilabu hiyo.

Suge Knight alipigwa risasi tumboni,kifuani na mkono wa kushoto.

Kwa sasa Suge Knight anakabiliwa na kesi ya mauaji baada ya kumgonga mtu na kutoroka.

Inadaiwa kile kilichotokea katika kisa hicho ndio sababu ya yeye kufanya vitendo kama hivyo.
Mwanamuziki Chris Brown



Alishtakiwa kwa kuwakanyaga watu wawili na kumuua mmoja huku mwengine akijeruhiwa vibaya.

Wakili wake anasema kuwa alikuwa akijaribu kuwatoroka washambuliaji .

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot