Mohammed Dewji ‘MO’ anogesha Simba Day, Ibrahim Hajibu atupia 2 za ushindi - MUANGALIZI

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, August 8, 2016

Mohammed Dewji ‘MO’ anogesha Simba Day, Ibrahim Hajibu atupia 2 za ushindi

Mo pamoja na baadhi ya viongozi wa Simba pamoja na wageni waalikwa wakiwapungia mikono mashabiki waliojitokea kushuhudia mechi kati ya timu hiyo dhidi ya Sports Club Villa

Mlezi na mnazi mkubwa wa Wekundu wa Msimbazi Simba Mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘MO’ amenogesha tamasha la timu kwa hali ya juu ambapo kila wakati wa mashambulizi baadhi ya mashabiki walikuwa wakiimba na kutaja jina la MO.
MO ambaye hadi sasa ameonyesha nia ya dhati ya kuitumikia klabu hiyo kama mfadhili mkubwa wapo katika mazungunzo ya hatua mbalimbali kufikia hali hiyo.
Timu ya Simba katika mchezo ambao pia unaendelea sasa dhidi ya Sports Club Villa, Wekundu hao wapo mbele kwa bao 2, zilizotupiwa kimiani na mchezaji wake Ibrahim Hajibu ambaye alitupia bao la kwanza kipindi cha kwanza na la pili katika kipindi cha pili tu cha mchezo huo.
Mlezi na mnazi mkubwa wa Wekundu wa Msimbazi Simba Mfanyabiashara Mohammed Dewji ‘MO’ akilishwa keki ya miaka 80 ya Wekundu hao wa Msimbazi
Wageni waalikwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, MO, na Dk. Kigwangalla

MO akisalimiana na mashabiki wa Simba baada ya mapunzimko.
 
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Hamisi Kigwangalla akilishwa keki hiyo ya miaka 80 ya Simba (Picha na Story ni kwa hisani ya Modewji Blog)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot